06 April, 2015
05 April, 2015
MVUA YAVUNJA MTANANGE KATI YA MTIBWA NA STAND UNITED
Hadi dakika ya 33 ya mchezo huo,
mwamuzi wa mtanange huo anapuliza kipyenga kiashilio kuwa mchezo
hautaendelea, Wenyeji Stand United walikuwa wakiongoza kwa bao 1-0,
ambapo Goli hilo lilifungwa na Haruna Chanongo kunako dakika ya 12.
Mbali na mchezo huo wa leo
kuvunjika, Pia jana Mtanange kati ya Simba na Kagera Sugar ulishindwa
kuchezeka baada ya Uwanja huo kujaa maji katika maeneo muhimu ya Uwanja
kama Laangoni na sehemu nyingine.
Kufatia uamuzi huo sasa timu hizo zitakutana kesho jumatatu endapo hari ya hewa itaruhusu.
MAGAZETINI LEO JUMAPILI>>>>>
NIPASHE
Askofu Gwajima anatakiwa kuripoti muda
wowote kuanzia leo katika Hospitali ya TMJ kwa uchunguzi zaidi baada ya
kuisha kwa muda ambao alipewa kwa ajili ya kupumzika.
“Tulimpa
muda wa wiki moja, hadi sasa muda umekwisha, hivyo wakati wowote
anatakiwa kuripoti Hospitalini ili kuangaliwa maendeleo ya hali yake na
kama haijaimarika, tutamchunguza zaidi”—Dk. Fortunatus Mazigo, daktari ambaye anamtibu Askofu huyo.
Daktari huyo amesema hawezi kuuzungumzia
ugonjwa ambao anaumwa Askofu huyo kutokana na maadili ya kazi yake, ila
akipata ruhusa kutoka kwa mhusika mwenyewe atafanya hivyo.
MTANZANIA
Ndoa ya Dk. Mengi ana Jacquiline Ntuyabaliwe ambayo ilifungwa kwa siri Mauritius ana kuhudhuriwa na marafiki wachache takribani 50 imezua gumzo.
Safari ya wawili hao kuelekea uchumba
ilianza Desemba mwaka 2014 ambapo walivalishana pete za uchumba katika
sherehe za kumbukumbu ya kuazaliwa ya Jacquiline iliyofanyika Dubai.
Rafiki wa karibu na Jacquiline, Nancy Sumari aliweka picha katika ukurasa wake wa Instagram ikimuonesha Jacquiline akirusha juu maua pamoja na rafiki zake akiwemo Faraja Kota, Nasreen Kareem na Sophia Byanaku.
Mengi na Jacquiline tayari wana watoto mapacha ambao nao pia walihudhuria ndoa ya wazazi wao.
MWANANCHI
Familia ya Diwani wa viti Maalum Mkoa wa Geita, Helena Mahona
imevamiwa na kushambuliwa na nyuki ambao wamejeruhi mama mmoja na
watoto wawili na kusababisha kifo cha mtu mmoja ambaye ni shangazi wa
Diwani huyo.
Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho, Joseph Majebele amesema alikuwa mbali na eneo hilo lakini akapewa taarifa ya kutokea kwa tukio hilo kwa njia ya simu na watu walioshuhudia.
Kamanda wa Polisi Geita, Peter Kakamba
amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa marehemu alifariki
hapo hapo kwenye tukio huku majeruhi wakikimbizwa Hospitai na hali zao
zinaendelea vizuri.
matokeo ya Borussia Dortmund vs Bayern Munich hapa
Wikiendi mbili zilizopita tulishuhudia vilabu mahasimu wa ligi za England Manchester UTD vs Liverpool na FC Barcelona va Real Madrid wakiumana – jana ilikuwa zamu ya Bundesliga – ambapo Borussia Dortmund waliwakaribisha wapinzani wao Bayern Munich katika dimba la Siguna Iduna Park.
Mchezo huo uliomalizika muda mfupi uliopita umeshuhudia Bayern wakipata ushindi mgumu wa goli 1-0 dhidi ya vijana wa Jurgen Klopp.
Robert Lewandoski mchezaji wa zamani wa Dortmund ndio aliyepeleka kilio kwa mashabiki wa timu yake ya zamani – baada ya kuunganisha kwa kichwa mpira uliokolewa na kipa wa Dortmund mapema katika kipindi cha kwanza.
Kwa matokeo hayo Bayern Munich wanaendelea kuongoza msimamo wa ligi kuu ya Ujerumani.
Matokeo mengine ya Bundesliga
Wayne Rooney anamagoli 185 kwenye Premier League,Andy Cole [187], Alan Shearer [260],#Epl Picha/Matokeo ya Man Utd dhidi ya Aston Villa.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7
KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...
-
Mpenzi msomaji wa safu hii ni siku nyingine tunakutana katika kujuzana,kukumbushana, na kuelimishana mila na desturi za makabila mbalimbal...
-
This is a song sang by a very gifted woman Adele, I sang it to show world that everyone appreciate and love to enjoy good music! Asa...
-
Mboga za majani na matunda zimekuwa zikisisitizwa kwa sana na wataalamu wa afya hasa kwa wanawake wajawaziti kwani zimekuwa zikiongeza Damu...