Hii ndio mara ya kwanza kwa ubalozi huo na haswa bendera ya Marekani kupepea tena nchini humo tangu mwaka wa 1961.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, John Kerry, aliyeko Havana ndiye aliyekuwa mgeni mheshimiwa katika dhifa hiyo ya kufungua upya ubalozi wa nchi yake nchini Cuba
Rais Obama na mwenzake wa Cuba Raul Castro walikubaliana mnamo December mwaka jana kuurudisha uhusiano wa kidiplomasia.
Marekani imelegeza baadhi ya vikwazo vya biashara na usafiri, hatahivyo bado vingine vingi vingalipo.
No comments:
Post a Comment