14 August, 2015

Ubalozi wa marekani wafunguliwa Cuba

Sherehe za ufunguzi wa ubalozi wa Marekani huko Cuba zimefanyika mjini Havana.
Hii ndio mara ya kwanza kwa ubalozi huo na haswa bendera ya Marekani kupepea tena nchini humo tangu mwaka wa 1961.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, John Kerry, aliyeko Havana ndiye aliyekuwa mgeni mheshimiwa katika dhifa hiyo ya kufungua upya ubalozi wa nchi yake nchini Cuba

Katika sherehe zilizofanyika Havana, Kerry aliandamana na wanajeshi watatu wa zamani ambao waliishusha bendera ya Marekani katika jengo la ubalozi huo mnamo 1961.
Rais Obama na mwenzake wa Cuba Raul Castro walikubaliana mnamo December mwaka jana kuurudisha uhusiano wa kidiplomasia.
Marekani imelegeza baadhi ya vikwazo vya biashara na usafiri, hatahivyo bado vingine vingi vingalipo.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...