18 October, 2016

ROMA apangua skendo za watoto nje ya ndoa

Msanii Roma Mkatoliki amempa zawadi ya wimbo mtoto wake anayeitwa Ivan katika siku yake ya kuzaliwa ambapo ametimiza miaka minne, lakini kuna tetesi kuwa rapa huyo ana mtoto mwingine nje ya ndoa.
Ukiongelea wasanii ambao wanafanya vizuri kwa upande wa hip hop huwezi kuacha jina la Roma Mkatoliki. 

eNewz ilipiga story na Roma na alisema kuwa hizo skendo hazikuanza leo kwa sababu tayari aliwahi kupata skendo ya yeye na aliyekuwa mtangazaji wa kipind cha TV cha Nirvana, Lotus Kyamba kuwa mtoto aliyenaye ni wa kwake licha ya kwamba siyo kweli na kwamba yeye ana mtoto mmaja pekee ambaye ni Ivan

“Mimi kiukweli nina mtoto mmoja tu wa kiume ambaye ni Ivan na hizo story za mimi kuwa na mtoto nje zipo niliwahi kuambiwa nina mtoto na lotus kumbe siyo kweli na huwa sipendi kuziongelea sana kwa sababu mimi nina mke wangu na nina mtoto mmoja tu ambaye ni Ivan”

CHANZO: EATV.TV

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...