Msanii wa Hip Hop kutoka Mwanza Young Killer amesema pete yake aliyoivaa
katika kidole chake ni urembo kama urembo mwingine kama miwani au
hereni na siyo ya kishirikina au ya bahati kama watu wanavyoidhania.
Akiongea ndani ya Kipindi cha eNewz Msodoki amesema amekuwa ni mtu mwenye bahati
kabla hata ya kuivaa pete hiyo au kuwa Young Killer hivyo pete hiyo
haihusiki katika mafanikio yake “hofu ndo ugonjwa wako na kama mtu
anafanya ushirikina ni imani yake imempelekea awe hivyo lakini kwa mimi
sina imani na mambo ya kishirikina japokuwa najua kuwa yapo” alisema
Msodoki.
Hata hivyo Msodoki alisema pamoja na mawazo ya watu kuhusisha pete
yake na mambo ya kichawi lakini yeye hawezi kuivua itaendelea kukaa
kidoleni kwake "... na kwa wale wanaoona tofauti waendelee tu kuwa na
imani yao kwa kuwa ni vyema kutafuta haki yako bila kumkwaza mwenzako"
alimalizia hivyo Young Killer
CHANZO: eatv.tv
21 October, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7
KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...

-
Mshambuliaji huyo wa umri wa miaka 26 ambaye amekuwa akichezea klabu ya Corinthians ya Ugiriki amechezea taifa lake mechi 27 na kuwafungi...
-
Brit Awads 2016 zimefanyika huko London ambapo mwanamuziki Adele ameondoka na tuzo nyingi zaidi katika nomination alizo kuwepo. Hizi hapa...
-
Mboga za majani na matunda zimekuwa zikisisitizwa kwa sana na wataalamu wa afya hasa kwa wanawake wajawaziti kwani zimekuwa zikiongeza Damu...
No comments:
Post a Comment