21 October, 2016

Nikki wa Pili aonesha utofauti wake na Joh Makini

Rapa Nikki wa Pili ambaye hivi sasa bado anafanya vizuri na wimbo wake wa 'Sweet Mangi' amefunguka na kusema kuwa kimuziki kati yake yeye na Joh Makini kwa mtazamo wake yeye anaona kuwa Joh Makini amemzidi mbali sana katika sanaa,
Kutokana na hilo, Nikki amewataka watu watambue kuwa Joh Makini ana kipaji kikubwa zaidi yake na uzoefu pia.

Nikki wa Pili alisema hayo kupitia kipindi cha 'Ngaz kwa Ngaz' na kusema kuwa Joh Makini yupo kwenye muziki muda mrefu, ana uzoefu mkubwa zaidi na amefanya mambo mengi ambayo yeye yamemrahisishia katika muziki.
"Kwanza Joh Makini ana experince kuliko mimi, halafu naweza kusema 'In terms of music' yeye ana ujaribu mkubwa kuliko mimi kwani amethubutu vitu vingi kuliko mimi ambavyo mimi kwangu baadaye nimevitumia kama 'Benefits'. Lakini Joh Makini Its all do respect, talent wise amenipita mbali kwa mimi ninavyotazama" alisema Nikki wa Pili
Chanzo: eatv.tv

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...