Msanii wa Bongo fleva Khadija Said Maige maarufu kama Kadjanito
amefunguka na kusema kuwa amepagawa na mapenzi ya Tresor Lisimo mchezaji
wa mpira ambaye ndiye anataka kufunga naye ndoa tarehe 29 mwezi wa 10
mwaka huu.
Kadjanito kupitia kipindi cha eNewz kinachorushwa na kituo cha Tv EATV anasema aliona amekaa peke yake
kwa muda mrefu hivyo ameamua kuwa mke wa mtu ili na yeye awe mwanamke
aliyekamilika sababu amempata mtu anayependana naye na mtu ambaye
wanaelewana.
"Nimeamua kufunga ndoa kwani nilikaa muda mrefu peke yangu
nikatafakari nikaona siyo kitu kizuri nikiwa kama msichana ambaye nina
'Inspire' watu wengi lazima kuna vitu nifanye ili niwe mwanamke kamili,
maana ukiwa peke yako mtu anaweza kukuchukulia labda huyu mtu muhuni
lakini mimi nimeamua kuwa mke wa mtu, najua ni kitu kikubwa lakini
haitanifanya mimi niache kazi zangu za muziki"
Ameendelea kusema "Nimeamua kufunga ndoa sababu nimeona nimepata mtu
ambaye tunapendana, ninaendana naye na ninampenda sana. Aisee mimi
nafunga ndoa ya Kikristu yaani jamaa nimemzimia mpaka nimeamua kumfuata
katika imani yake, kiukweli ninamfuata" alisema Kadjanito
26 October, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7
KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...

-
Mshambuliaji huyo wa umri wa miaka 26 ambaye amekuwa akichezea klabu ya Corinthians ya Ugiriki amechezea taifa lake mechi 27 na kuwafungi...
-
Brit Awads 2016 zimefanyika huko London ambapo mwanamuziki Adele ameondoka na tuzo nyingi zaidi katika nomination alizo kuwepo. Hizi hapa...
-
Mboga za majani na matunda zimekuwa zikisisitizwa kwa sana na wataalamu wa afya hasa kwa wanawake wajawaziti kwani zimekuwa zikiongeza Damu...
No comments:
Post a Comment