24 October, 2016

Beki wa Manchester United Eric Bailly aumia vibaya

Beki wa Manchester United anayetoka Ivory Coast Eric Bailly alipata jeraha mbaya ya goti wakati wa mechi ambayo timu yake ililazwa 4-0 na Chelsea Jumapili.

Mchezaji huyo wa miaka 22 aliumia baada ya kukabiliana na Eden Hazard wa Chelsea.
ALiondolewa uwanjani dakika ya 52.

"Nina wasiwasi kwamba ni jeraha mbaya," meneja wa United Jose Mourinho alisema. "Ameumia kwenye goti, eneo lenye kano. Anahisi kwamba ni jeraha mbaya sana."

Bailly alikuwa amechezea United mechi zote walizocheza msimu huu ligini.
Alijiunga nao kutoka klabu ya Villarreal ya Uhispania kwa £30m kabla ya kuanza kwa msimu.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...