31 December, 2015

Ubelgiji yahofiwa kushambuliwa


Ubelgiji imesitisha sherehe za kijadi za kuwasha fataki mjini Brussels katika mkesha wa mwaka mpya, kwa hofu ya shambulizi.
Meya wa mji wa Brussels, Yvan Mayeur, amesema uamuzi huo umechukuliwa baada ya kufanywa kwa tathmini.
Mwanzoni mwa wiki hii, watu wawili walikamatwa nchini humo kwa kushukiwa kutaka kupanga shambulizi mjini Brussels katika mkesha wa mwaka mpya.
Ubelgiji imekuwa katika tahadhari ya hali ya juu tangu kutokea kwa shambulizi la kigaidi nchini Paris mwezi uliopita.
Baadhi ya wanaoshukiwa kuhusika na shambulizi hilo wapo nchini Ubelgiji.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...