15 October, 2015

Upinzani wapinga matokeo ya uchaguzi Guinea


Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini Guinea amejiondoa katika uchaguzi uliofanyika nchini humo akisema kuwa kulikuwa na udanganyifu mkubwa uliotekelezwa na serikali kulingana na kiongozi wake wa kampeni.
Uamuzi huo wa Cellou Diallo wa kujiondoa unajiri wakati ambapo matokeo yanaonyesha kwamba rais Alpha Conde anaongoza kwa wingi wa kura akitafuta kushinda awamu ya pili ya miaka mitano.
Wachunguzi kutoka muungano wa Ulaya wanasema kuwa uchaguzi huo ulikuwa wa haki licha ya matatizo makubwa ya vifaa.
Matokeo kamili ya uchaguzi huo yanatarajiwa mwishoni mwa wiki hii.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...