15 October, 2015

Kizza Besigye akamatwa Uganda


Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda, Kizza Besigye amekamatwa pamoja na wanachama wengine wa chama chake.
Kukamatwa kwao kunajiri wakati ambapo chama hicho kilikuwa kinaanza kampeni zake kwa uchaguzi mkuu wa mwaka ujao kulingana na mwandishi wa BBC Patience Atuhaire katika mji mkuu wa Kampala.
Watu wengine wawili pia walikamatwa pamoja na bwana Besigye wakati maafisa wa polisi walipovamia nyumba yake mapema leo kulingana na vyombo vya habari.
Mbunge wa chama hicho Ssemujju Nganda ambaye pia ni msemaji wa chama hicho pia alikamatwa nyumbani kwake na amepelekwa katika kituo cha polisi cha Naggalama,karibu na mji mkuu wa Kampala.
Besigye amepoteza mara tatu kwa rais Yoweri Museveni katika uchaguzi uliokumbwa na utata.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...