28 August, 2015

Wapenzi wa jinsia moja wadai kunyanyaswa


Kundi la kuteta haki za kibinadam nchini Tanzania la LGBTI Voice of Tanzania imetangaza kuwa imeanzisha kampeini ya kuchangisha pesa za kututea haki za wapenzi wa jinsia moja, watu walio badili jinsia zao.
Shirika hilo limesema kuwa sheria za Tanzania zinawakandamiza watu wanaoshabikia mapenzi ya jinsia moja.
Mkurugenzi wa shirika hilo James Wandera amesema wamechangisha zaidi ya dola elfi thelathini, has kutoka wa wafadhili kwa njia ya mtandao.
Amesema wanapanga kutumia fedha hizo kuzuia uwezekano wa wabunge kuidhinisha mswada uliowasilishwa bungeni.
Mswada huo haujajadiliwa bungeni lakini unapendekeza adhabu ya dhidi ya wapenzi wa jinsia moja kuimarisha zaidi.Sheria za Tanzania zimeharamisha mapensi ya jinsia moja na wale wanaopatikana na hatia hupewa adhabu ya kifungo cha hadi miaka 20 gerezani.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...