28 August, 2015

STARS YASHINDWA KUTAMBA UTURUKI MBELE YA LIBYA, BOCCO AFUNGA GOLI LA KUFUTIA MACHOZI

Kikosi cha Stars kilichoanza leo dhidi ya Uganda 
Timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imeshindwa kutamba mbele ya Libya baada ya kufungwa kwa goli 2-1 kwenye mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu kuelekea mechi yake dhidi ya Nigeria kuwania kufuzu kucheza mashindano ya Mataifa ya Afrika yatakayofanyika mwaka 2017 huko Gabon.
Mchezo huo uliochezwa nchini Uturuki ambako Stars imeweka kambi, ulikuwa ni wa mazoezi na ulikuwa hautambuliwi na CAF wala FIFA ila ulikuwa unatumiwa na makocha wa timu zote mbili kwa ajili ya kutathmini vikosi vyao kuelekea michuano ya kutafuta tiketi ya kushiriki michuano hiyo ya Afrika.
Kwenye mchezo huo, goli pekee la Tanzania limefungwa na John Bocco ‘Adebayor’ kwa mkwaju wa penati baada ya Simon Msuva kufanyiwa madhambi kwenye eneo la hatari na mwamuzi kuamuru ipigwe penati ndipo Bocco akaipatia Stars goli la kufutia machozi.
Stars bado inaendelea na kambi yake nchini humo ambapo ikirejea jijini Dar es Salaam itafanya maandalizi kwa siku chache kabla ya kuivaa Nigeria Septemba 5 mwaka huu kwenye uwanja wa Taifa.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...