28 August, 2015

DE BRUYNE HUYOOO EPL YAMEBAKI MASAA TU, KUJIUNGA NA WAKALI HAWA…

De Bruyne KelvinMachester City wamemuwekea mezani bonge la mshahara kiungo wa Wolfsburg Kevin De Bruyne, mkurugeni wa michezo wa timu hiyo Klaus Allofs amewaambia waandishi wa habari.
Akizungumza mjini Monaco wakati wa kupanga makundi ya UEFA Champions League, amesema makubaliano kati yao na Man City yanakaribia kukamilika. Amefafanua kuwa dili hilo litakalovunja rekodi ya klabu hiyo kwa kumuuza De Bruyne kwa kitita cha pauni milioni 54 linaweza kukamilika ndani ya masaa 48 baada ya makubaliano ya pande mbili kufikiwa.
Mgurugenzi huyo wa Wolfsburg amesema, ofa kutoka Man City imekuwa kubwa mno na wao hawawezi kupambana kuwazuia.
“Tumekuwa kwenye mazungumzo na sasa tumekaribia kukamilisha lakini dili bado halijakamilika. Lakini nadhani tutafikia muafaka muda si mrefu”.
Allofs amesema, timu yake haiwezi kushindana na matajiri hao wa EPL ambao wameahidi kumpa De Bruyne mshahara wa pauni 200,000 kwa wiki kiungo huyo mwenye miaka 24.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...