28 August, 2015

Askofu aliyekabiliwa na kesi aaga dunia



Aliyekuwa Askofu wa kanisa la Katoliki kutoka Poland, ambaye alitarajiwa kufikishwa mahakamani kwa madai ya dhuluma za ngono amefariki.
Jozef Wesolowski alipelekwa hospitali mwezi uliopita, saa chache tu kabla ya kufishwa mahakamani.
Askofu huyo anatuhumiwa kuwapa watoto pesa na kuwadhulumu kingono wakati alikuwa balozi wa Vatican katika Jamuhuri ya Domincan.
Kamati maalum ya kanisa la Katoliki ilimpata na hatia na ikamsimamisha kazi mapema mwaka huu.
Wesolowski angelikuwa mtu wa kwanza wa ngazi ya juu katika kanisa hilo la Katoliki kufikisha mahakamani mjini The Vatican kwa madai ya kuwadhulumu watoto kingono.
BBC

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...