14 July, 2015

Shirikisho la soka la Urusi limethibitisha kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba na kocha mkuu wa timu ya Taifa ya nchi hiyo

18E4B25E000005DC-0-image-a-2_1435161204487
Shirikisho la soka la Urusi limethibitisha kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba na  kocha mkuu wa timu ya Taifa ya nchi hiyo, Fabio Capello   baada ya kushindwa kutimiza malengo waliyojiwekea.
Katika taarifa yake, RFU wamemshukuru  Capello kwa kazi yake aliyofanya na wamemtakia kila la kheri katika maisha yake yajayo, huku naye akilishukuru Shirikisho hilo, mashabiki pamoja na wachezaji kwa kutoa ushirikiano mkubwa katika kipindi chote alichofundisha timu hiyo.
Mkataba wa Capello unatakiwa kumalizika mwaka 2018 ambapo Urusi itahodhi kombe la Dunia, lakini maamuzi yaliyochukuliwa yanalifanya Shirikisho hilo limlipe fidia ya paundi milioni 11.
Ripoti kutoka Urusi zinasema kwamba,  kocha wa CSKA Moscow, Leonid Slutsky anapewa nafasi kubwa ya kurithi mikoba ya Capello mwenye umri wa miaka 67 ambaye amekinoa  kikosi cha Urusi kwai kwa miaka mitatu.
Capello alianza kuifundisha Urusi mwaka 2012, muda mfupi baada ya kujiuzulu kuifundisha  timu ya Taifa ya England, lakini alishindwa kuwaongoza vizuri Warusi katika fainali za kombe la Dunia mwaka jana nchini Brazil na mwaka huu nchi hiyo imefanya vibaya katika mechi za kufuzu kombe la Mataifa ya Ulaya 2016.
Urusi inashika nafasi ya tatu katika msimamo wa kundi G ambapo imeshinda mechi mbili tu kati ya sita ilizocheza.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...