01 July, 2015

Radamel Falcao amesaini mkataba wa kujiunga na klabu ya Chelsea

Falcao 1
Radamel Falcao amesaini mkataba wa kujiunga na klabu ya Chelsea na ataungana na timu yake mpya kwenye ziara ya kujiandaa na msimu ujao (pre-season) huko bara la America ya Kaskazini hii ni kwa muji wa ripoti.

Mjomba pamoja na baba yake Falcao wamethibitisha kwamba, mkataba umeshasainiwa kati ya mshambuliaji huyo na klabu ya Chelsea.
Kwa mujibu wa gazeti la The Guardian, Chelsea wamekubaliana na Monaco kumsajili Falcao kwa mkopo wa mwaka mmoja lakini mkataba huo unakipengele cha kumsajili moja kwa moja msimu ujao.
Chelsea bado hawajatangaza rasmi kumsajili Falcao lakini walikuwa na mazungumzo na wakala wa mchezaji huyo, Jorge Mendez kwa takribani wiki tatu ili kuhakikisha wanamsajili Falcao licha ya kwamba mshahara wake unagharimu kiasi cha pauni 265,000 kwa wiki.
The Guardian limeripoti kuwa, mabingwa hao wa ligi ya England wakotayari kumlipa Falcao kitita cha pauni 180,000 kwa wiki na pauni milioni 4 kama ada ya uhamisho.
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amesema atamsaidia Falcao kurudia makali yake ya zamani baada ya kuwa na msimu mbovu alipokuwa Manchester United kufuatia jeraha la goti la mudamrefu.

Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...