01 July, 2015

Evans Aveva:Hamis Kiiza atapimwa na kusaini mkataba kuitumikia Msimbazi.

Hamis Kiiza of Uganda tries to go past Amandio Da Costa of Angola during the 2014 World Cup Qualifier football match between Uganda and Angola at the Mandela Stadium, Namboole, Kampala on 15 June 2013 ©Ismail Kezaala/BackpagePix
RAIS wa Simba, Evans Aveva, amesema mshambuliaji aliyetemwa Yanga, Hamis Kiiza atawasili nchini wakati wowote na kpimwa afya kabloa ya kusaini mkataba kuitumikia klabu hiyo ya Msimbazi.
Aveva, aliyekuwa amefuatana na makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ katika hafla ya uzinduzi wa kadi ya watoto ya uanachama wa Simba jijini hapa leo mchana, amesema wamefikia hatua nzuri na mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu ya URA ya Uganda.
“Mazungumzo yetu na Kiiza yamekwenda vizuri, muda wowote kuanzia leo (jana) atawasili nchini kwa ajili ya kupimwa afya. Akifuzu vipimo vya afya, tutamsajili kuwa miongoni mwa wachezaji wetu,” amesema Aveva.
Ingawa kiongozi huyo wa juu wa Simba hakutaja muda wa mkataba ambao Kiiza atasaini, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu hiyo, Zacharia Hanspope amesema leo kuwa nyota huyo atatia saini ya kandarasi ya miaka miwili.
“Sisi na Kiiza kila kitu safi, anakuja kusaini miaka miwili hapa,” ametamba Hanspope.
Kiiza aliachwa na Yanga Desemba mwaka jana ili kumpisha mshambuliaji Mliberia Kpah Sherman baada ya kuitumikia klabu hiyo tangu 2011.
Tangu atemwe na mabingwa hao mara 25 wa Tanzania Bara, Mganda huyo anayetisha kwa kupachika mabao, amekaa bila timu baada ya mpango wake wa kwenda kucheza Fanja ya Oman kushindikana Januari mwaka huu.
 
Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...