05 July, 2015

HATIMAE CHILE NDIO MABINGWA WAPYA COPA AMERICA YAIFUNGA ARGENTINA PENALTI 4 KWA 1 (VIDEO YA PENALT ZOTE)

Sanchez 2Penati ya Alexis Sanchez imewapa Chile ubingwa wa Copa America kwa mara ya kwanza kwenye mchezo wa fainali kali na ya kusisimua iliyopigwa usiku wa Jumamosi kati ya wenyeji Chile dhidi ya Argentina na Chile kunyakuwa kombe hilo kwa penati 4-1.Sanchez 4Ilibidi mikwaju ya penati iamue nani atanyanyua ndoo hiyo baada ya kushuhudia dakika 90 za mtanange huo zikimalizika bila timu yoyote kuzifumania nyavu za mpinzani wake. Zikaongezwa dakika 30 ambazo pia zilimalizika bila kumpata mbabe wa pambano hilo ndipo mikwaju ya penati ilipotumika kuamua nani ataondoka na mwali huyo aliyekuwa akigombewa na Mataifa ya 12 ya America Kusini.
Sanchez 3 
Mchezo ulikuwa ni mkali na wa kasi, timu zote zilijitahidi kutengeneza nafasi na kufanya mashambulizi kadhaa lakini milango yote miwili ilikuwa migumu kuruhusu nyavu kutikiswa na washambuliaji wa timu zote mbili.
 Kombe hilo linawafanya Chile wamalize ukame wa mataji nchini kwao hasa kwenye mchezo wa soka kwasababu walikuwa hawajawahi kutwaa taji lolote kubwa la kimataifa.
Mchezaji nyota wa FC Barcelona Lionel Messi, ameshindwa kutwaa taji kwa mara nyingine kwenye fainali yake ya pili akiwa na Argentina baada ya mwaka jana (2014) kulikosa kombe la dunia mbele ya Ujerumani kwenye fainali za kombe hilo ilizofanyika nchini Brazil.Messi 1Messi ameshashinda mataji yote kwenye ngazi klabu, lakini ameshindwa kutwaa taji lolote akiwa ametinga uzi wa Argentina.HiguainMatias Fernandez, Arturo Vidal, Charles Arangui na Alexis walifunga mikwaju yao ya penati wakati wachezaji waliokosa penati kwa upande wa Argentina ni Gonzalo Higuain ambaye alipaisha juu wakati golikipa wa Chile Claudio Bravo alipangua mkwaju wa penati uliopigwa na Ever Banega huku Messi akiwa ni mchezaji pekee aliyefunga penati ya Argentina.
Matias Fernandez, Arturo Vidal, Charles Arangui na Alexis walifunga mikwaju yao ya penati wakati wachezaji waliokosa penati kwa upande wa Argentina ni Gonzalo Higuain ambaye alipaisha juu wakati golikipa wa Chile Claudio Bravo alipangua mkwaju wa penati uliopigwa na Ever Banega huku Messi akiwa ni mchezaji pekee aliyefunga penati ya Argentina. NMEKUWEKEA VIDEO YA PENALTI ZOTE BONYEZA PLAY KUZITAZAMA>>>>>>>>>

 Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...