01 July, 2015

Manchester United imetenga dau la Euro milioni 160 kwa ajili ya kumnasa mshambuliaji wa Bayern Munich Thomas Muller.

MullerHabari kubwa imeripotiwa na mwandishi Christian Falk kuwa, klabu ya Manchester United imetenga dau la Euro milioni 160 kwa ajili ya kumnasa mshambuliaji wa Bayern Munich Thomas Muller.

Kwa muji wa ripoti hiyo, Man United imetoa ofa hiyo kwa Muller kwa ajili ya kumsajili na kumpa mkataba wa miaka mitano kuitumikia klabu hiyo ya Old Trafford. Mashetani wekundu wameweka kitita hicho cha Euro milioni 160 ikiwa ni ada ya uhamisho pamoja na mshahara wa mchezaji huyo.
Capture 1
Christian Falk ametoa taarifa hiyo kufuatia mahojiano aliyofanya na Muller kwa ajili ya gazeti la udaku linaloitwa ‘Bild’ ambapo gazeti hilo linasema kuwa Man United imependekeza dili hilo kwa Muller ambaye mwaka jana alitwaa kombe la dunia akiwa na timu yake ya taifa ya Ujerumani.
Taarifa hizo za Manchester United kupeleka ofa hiyo kwa ajili ya kumnasa Muller kutasababisha baadhi ya mashabiki waamini kuwa klabu hiyo inaweza ikamnyakua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25.
Capture 2
Kuondoka kwa Radamel Falcao na tetesi za Robin van Persie kutaka kutimka ndani ya kikosi hicho, kutapelekea Wayne Rooney kuwa mshambuliaji pekee ambaye anatazamwa na Manchester United kuelekea msimu ujao.
Sasa je,Manchester wangependa kumsajili Muller? Ndiyo wanataka. Lakini je, wataweza? Ni kitu ambacho kinaoinekana kwa sasa kinaonekana kuwa kigumui.

Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...