07 July, 2015

Bondia asiyepigika, Floyd Mayweather amevuliwa mkanda wa ubingwa wa WBO

Image result for Floyd Mayweather

Bondia asiyepigika, Floyd Mayweather amevuliwa mkanda wa ubingwa wa WBO, uzito wa Welterweight  unaohusisha kilo 67 na 77 ambao alishinda mwezi Mei mwaka huu dhidi ya Manny Pacquiao kutokana na  kushindwa kufuata sheria na kanuni za Shirikisho hilo.
Kamati ya mashindano ya WBO imesema kwamba haina jinsi ya kufanya zaidi ya kumvua mkanda huo Mayweather ambaye ameshindwa kulipa ada kutoka kwenye pambano alilopigana na Pacquiao.
Ijumaa iliyopita, ilikuwa siku ya mwisho kwa  Mayweather kutimiza vigezo vya ubingwa wa WBO ikiwemo kulipa ada ya dola laki mbili kutoka katika pambano lake na Pacquiao pamoja na kujivua ubingwa wa uzito wa light-middleweight wa WBC na WBA.
Mayweather  anayetajwa kuwa mwanamichezo tajiri zaidi Dunianiameshindwa kutelekeza agizo hilo, hivyo kamati imeamua kumvua mkanda  wake wa kwanza wa WBO.
Bondia Timoth Bradley Jr anatarajiwa kupewa mkanda huo baada ya mwezi uliopita kumpiga kiutata,  Jessie Vargas  katika pambano la kutafuta bingwa wa muda wa uzito huo, ingawa Mayweather mwenye umri wa miaka 38 amepewa siku 14 za kukata rufaa.
Mayweather bado anashikilia ubingwa wa welterweight na super-welterweight  wa WBC na  WBA,  ingawa kisheria,  bondia haruhisiwi kushika ubingwa wa dunia kwa madaraja mbalimbali.

Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...