19 June, 2015

stori zote za magazeti zilizosikika leo Ijumaa June 19 2015 hapa. (Audio)

19Jaji mkuu wa zamani Augustine Ramadhani azua mjadala kwa wagombea urais CCM baada ya kuchukua formu ya ugombea urais kupitia chama hicho na mwandishi wa TBC Florence Diyauli afariki dunia jana June 18 akiwa amelazwa hospitali kwa ajili ya matibabu.

Mashine ya BVR zalipua moto mkoani Arusha, chama cha CHADEMA mkoa wa Arusha leo kufanya maandamano makubwa kupinga hujuma katika uandikishaji wananchi katika daftari la kudumu.
Kuna stori nyingine imesikika leo kutoka mkoani Mara ambako mtoto wa miaka 12 Penina Joseph ageuka bubu baada ya kung’atwa na mamba mwaka jana akiwa mtoni anachota maji.
Stori nyingine inatoka nchini Kenya ambako Gavana wa Benki kuu ya Kenya Patrick Ngoroje mwenye umri wa miaka 54 azua mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii baada ya kusema kua hajaoa mpaka sasa licha ya umri kumtupa mkono, Gavana huyo aliibuka kidedea baada ya kuchaguliwa na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta  kua Gavana wa Benki Kuu ya nchi hio mwaka huu.
Hapa chini iko sauti ya stori zote hizi bonyeza play kuzisikiliza.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...