30 June, 2015

Ramos amefanya uamuzi huu

Wiki moja baada ya ofa ya kwanza ya Manchester United kumsajili Sergio Ramos kukataliwa na Real Madrid, hatimaye mchezaji huyo ambaye yupo mapumzikoni ametoa kauli yake United walituma ofa ya kwanza ya paundi millioni 28.3 kwa Madrid ili kupata saini ya beki huyo wa kimataifa wa Spain, lakini Madrid waliikata ofa hiyo.
Hata hivyo baada ya Ramos kugundua Madrid wameikataa ofa hiyo, alichukua uamuzi wa kuwaweka wazi viongozi wa Madrid kupitia wakala wake kwamba – Anataka kuondoka na kujiunga na United na kuiomba Madrid ikubaliane bei na Manchester United. Uamuzi huo wa Ramos umeishtua Madrid, ambao walitegemea wangefanya makubaliano ya mkataba mpya na beki huyo. Madrid wanategemewa kujaribu kumtuliza Ramos na mkataba mnono mpya lakini kaka na meneja wa mchezaji huyo – Rene Ramos ameshaifahamisha Madrid lengo la mteja wake kutaka kuanza maisha mpya sehemu nyingine.
Rene ameripotiwa kusema kwamba Ramos anataka kuhamia Old Trafford wakati huu wa dirisha la usajili na klabu pekee ambayo anataka Madrid ifanye nayo makubaliano ni United.

Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...