01 June, 2015

Mbunge Augustino Mrema amelalamika tena kuhusu yaliyosemwa Jimboni kwake Vunjo !!

Voting
Ni zaidi ya mara mbili nasikia Mbunge wa Vunjo, Augustino Mrema akilalamika kuhusu kufanyiwa fitna na watu kwenye Jimbo lake la Vunjo, leo katika Kikao cha Bunge Dodoma amepewa nafasi tena.. kawasha kipaza sauti, kalalamika tena kuhusu anachofanyiwa Jimboni kwake.
Mimi pale Jimbo la Vunjo Shule ya Muungano iliungua, nilitoa Mil.21 kwenye mfuko wangu wa Mbunge ili kusaidia, mbona sioni Wizara mmetenga shilingi ngapi?
Mwisho akaja Katibu Mkuu wa CCM, na nyie CCM mmeanza kushiriki katika uongo.. Katibu Mkuu badala ya kwenda kuwapa pole kwenye Jimbo langu anasema ‘kila Jimbo lina mfuko wa Mbunge ambao ni Mil. 25 kwa miezi mitatu, kwa mwaka ni Mil.100, hamuwezi kuwa na Kiongozi ambae ni Mbunge na wakati huohuo ndie Mwenyekiti wa Mfuko huo, je si atajipendelea?’.. Naomba niulize Serikali, ni kweli Vunjo tumepata Mil. 400 kama alivyosema Kinana au mnanipakazia?
Kwa nini mnakuja kwangu mnasema maneno ya uongo nyie CCM? Kwa nini CCM mnanichangia kama mpira wa kona kule Vunjo? Kwa nini mnajiunga na Wapinzani kwa kusema maneno ya uongo?
Mlizonipa ni Mil.150 lakini mnaenda Vunjo mnawaambia watu nimechukua Mil. 400, naomba katika Mil. 400 mtoe hizo Mil.150 mnipe hiyo chenji tena leo hii
Kwa nini mnaenda kusema hivyo jamani mna ajenda gani na mimi? Uongo huu umenisononesha, na mimi nataka niwaambie CCM kwamba habadilishwi mtu kule Vunjo. Hizi mbinu zinazotumika kunidhoofisha.. Nataka chenji yangu nikafanye nayo Kampeni
 Msikilize mwenyewe Mbunge Mrema wakati akilalamikia ishu hiyo leo Bungeni Dodoma.>>>>>

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...