13 June, 2015

AZAM FC leo imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Ame Ally ‘Zungu

10407996_905036169559101_6675452961550561514_n
Ame (kushoto) baada ya kusaini Azam fc
AZAM FC leo imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Ame Ally ‘Zungu’ na kumsainisha mkataba wa miaka miwili.
Makamu mwenyekiti wa Azam fc, Nassor Idrissa ‘Father’ amethibitisha kuinasa saini ya Ame na kusema wameshamalizana na klabu ya Mtibwa.
Idrissa ameongeza kuwa Straika huyo aliwavutia kwa kiwango chake cha juu msimu wa 2014/2015 akiwa na Wakata miwa wa Manungu  na wanaamini chini ya kocha mkuu Stewart Hall anaweza kuisaidia Azam kuliko alivyoisaidia Mtibwa Sugar.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...