13 June, 2015

UGANDA ‘The Cranes’ imeitandika 2-0 Botswana

Geoffrey-Massa-150609-KicksBall-BPP300
UGANDA ‘The Cranes’ imeitandika 2-0 Botswana katika mechi ya ufunguzi ya kundi D kuwania kufuzu kombe la mataifa ya Afrika (Afcon 2017) iliyopigwa  leo uwanja wa Nelson Mandela, Namboole, mjini Kampala.
Magoli ya Uganda yamefungwa na Geoffrey Massa dakika ya 55′ na Mshambuliaji wa zamani wa Azam fc, Brian Umony katika dakika ya 66′.
Uganda waliingia kwenye mechi hii wakipewa nafasi kubwa ya kushinda kutokana na rekodi nzuri ya hivi karibuni hususani mechi za kufuzu.
Kabla ya mechi ya leo Uganda walikuwa wemeshinda mechi 7 kati ya 7 walizocheza za kufuzu katika uwanja wa nyumbani.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...