05 May, 2015

YANGA NA AZAM PATACHIMBIKA JUMA TANO

tiboloha
Kesho Jumatano saa kumi jioni katika tasnia ya Kabumbu nchini wapenda soka macho na masikio yao yatakuwa katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam kushuhudia Mtanange wa Mabingwa wapya wa VPL Yanga SC pamoja na Mabingwa waliokuwa watetezi  Azam FC huku
kukiwa na dua mbalimbali za timu nyingine zikiombea neema upande mmoja na Kuomba zahama kwa upande wa pili.
Bila shaka katika Mtanange huo Simba watakuwa wakiishangilia Yanga ili iweze kushinda dhidi ya Azam ili waweze kujiwea pazuri katika kuwania nafasi ya pili ambayo pia Azam wanaitaka kwa udi na ubani, Azam wao watakuwa wakiomba ili waweze kushinda na kujihakikishia ushiriki wa michuano ya kimataifa hapo mwakani.
Kuelekea mtanange huo Shaffihdauda.com imezungumza na viongozi wa timu zote mbili, Katibu mkuu wa Yanga Dk Jonas Tiboloha pamoja na Meneja wa Azam FC Jemedali Said ambapo kila mmoja amesema mchezo huo wanauchukulia kama fainali kwani ni muhimu kwao, Yanga ikitaka kukabidhiwa kombe lao kwa heshima ya kutofungwa na aliyekuwa bingwa mtetezi, Huku Azam wakitaka kushinda ili wapate nafasi ya ushiriki wa michuano ya kimataifa Afrika hapo mwakani.
Jemedali Said amesema kuwa baada ya kufungwa na Simba waliendelea na mipango ya timuwachezaji wakiwa kambini kwa kutambua umuhimu wa Mchezo.jemedali
“Ndio Tunaelekea mchezo na Yanga na maandalizi yetu yako vizuri kama ambavyo tumekuwa tukifanya siku zote kwasababu hata kabla hatujacheza na Simba tulikwisha amua kwamba timu itakaa kambini hadi hapo ligi itakapokuwa imekwisha, Baada ya kupoteza na Simba siku ya Jimapili timu imerejea ambini na jana imefanya mazoezi jioni na leo itafanya mazoezi jioni tayari kwa mchezo wa kesho, Kwahiyo sisi kama Timu tumejiandaa tunajua ni moja kati ya mechi ngumu kabisa, Hatujawahi kucheza na Yanga alafu mechi ikawa nyepesi siku zote mechi inakuwa ngumu”
“Muda huu ugumu unaongezeka kwasababu tayari Yanga wamekwisha kabidhiwa ubingwa sisi kesho tutakacho kifanya ni kwaajiri ya mabingwa kama itakavyokuwa, Tunaamini kuwa matokeo yake yakiwa mazuri kwetu itakuwa ni faida kwasababu tutakuwa tumepata nafasi ya kwenda kushiriki michuano ya kimataifa kwa mara nne mfurulizo, Lakini tunajua ugumu uliopo wa kupata matokeo hayo ambayo sisi tunayategemea” Amesema Jemedali Said Meneja wa klabu ya Azam FC.ngassa azam
Kwa upande wa Yanga ambao tayari kulikuwa na uvumi kuwa watachezesha wachezaji wa kikosi cha pili na kuwapumzisha nyota wao kwasababu tayari wamekuwa mabingwa,Dr. Tiboloha amekanusha vumi hizo kwa kusema watapambana mwanzo mwisho ili kuondoa aibu ya kufungwa na bingwa mtetezi.
“Labda nikuhakikishie tu kitu kimoja cha siri kwamba, Nilisema wiki mbili zilizopita nilipokuwa nikilalamikia ratiba ya ligi na ninaendelea kusema tena leo,  Yanga hatuta pumzika, tutapumzika Ligi ikimalizika baada ya mchezo wa Ndanda FC, Kwamaana hiyo sisi tutaingiza kikosi chetu kamili kesho kwa maana hiyo kila mchezaji ambaye yupo fit atacheza, Na nimechi ambayo sisi tumedhamilia kushinda kwasababu haitaleta maana yoyote kwa watu tumesha kuwa mabingwa alafu twende tukafungwe na mtu aliyekuwa bingwa tetezi ambaye tumemnyanganya ubingwa,”
“ Kwa maana hiyo tunaingia tukiwa tumedhamilia kushinda na tunajua mechi ni ngumu na tunaingia tukiwa tunawaheshimu kama tulivyokuwa tunawaheshimu timu nyingine zilizopita, Tunajua Azam ni timu ambayo imeundwa vizuri, inawachezaji wazuri, inacheza mpira mzuri achilia matokeo ambayo walikuwa wanayapata hivi karibuni lakini sisi tukiangali wanaupande mzuri sana kwahiyo ni mechi ambayo hatuta legea kwa kitu chochote kile na kwa namna yoyote ile, kwahiyo tunaenda kucheza tukijua ni lazima tuondoke tukiwa tumeshinda mchezo huo” Amesema Katibu huyo wa Yanga Dr. Tiboloha.yanga jjjj
Kwa upande wa Jemedali Said Meneja wa Azam FC alipotakiwa kuelezea changamoto zilizopelekea kufanya vibaya kwa msimu huu ikiwa hata katika michuano ya klabu Bingwa kuondolewa mapema alijibu kama ifuatavyo.
“Ni kweli kwamba ukiangalia msimu huu ulivyokuwa ukilinganisha na timu ilivyokuwa msimu uliopita ni dhahiri kwamba hatujafanya vizuri, Hatujafanya vizuri kwa maana kwamba, kwanza hatujafika mbali kwenye mashindano ya kimataifa Champions league tumetolewa raundi ya mwanzo, Marengo yeu ya pili ilikuwa kutetea Ubingwa kwahilo tumefail pia maana Yanga wamechukua, Lakini kwakuwa msimu haujaisha leo niseme wapi tumejikwaa na nini kimesababisha nadhani itakuwa bado mapema mno sisi bado tunamichezo miwili”
“Utaratibu ambao sisi tumejiwekea ni kwamba kuna sehemu kama tatu ambazo zinatoa ripoti ya msimu mzima ulivyokuwa , Benchi la Ufundi kupitia kwa mwalimu mkuu aliopo sasa George Nsimbe Best ataleta ripoti yake, mimi pia kama meneja nina Ripoti yangu pia Utawara kwahiyo zote zikisha jumlishwa ndio tunajua nini kwa msimu mzima tunarekebisha, Kwahiyo mwisho wa msimu ndio nitatoa jibu la mapungufu yalikuwa yapi” Amesema Jemedali Said.azam (1)imu hizo mbili kesho zitakutana katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam kucheza mchezo wao ambao ni kipolo, lakini tukio kubwa baada ya kumalizika kwa mchezo huo Bodi ya ligi pamoja na Wadhamini wa ligi ambao ni Vodacom watawakabidhi Yanga kombe lao la Ubingwa ambao wameuchukua Msimu huu wa 2014/15 wakiwapokonya Azam FC waliouchukua mwaka jana.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...