04 May, 2015

V Persie anyimwa haki za kupiga Penalti


Mkufunzi wa kilabu ya Manchester United Louis Van Gaal amempokonya mshambuliaji wa kilabu hiyo Robin Van Persie haki za kupiga mkwaju wa penalti baada ya kukosa mkwaju kama huo katika mechi dhidi West Brom.

Alipoulizwa iwapo Van Persie angeendelea kama mchezaji aliyeorodheshwa kupiga penalti kwa niaba ya kilabu hiyo alijibu ''hapana,amefika mwisho wake.Kila mara anarejelea makosa hayo hayo aliongezea''.
''Wayne Rooney pia amekosa mkwaju wa penalti na unapokosa mkwaju huo basi ujue utapiga foleni''.,aliongezea
Ushindi wa West Brom ulikuwa matokeo mabaya kwa upande wa Manachester United kwa mara ya tatu mfululizo.
Van Persie mwenye umri wa miaka 31 alikuwa na fursa ya kusawazisha kufuatia bao la Chris Brunty kunako dakika ya 63 baada ya refa Anthony Taylor kumpata na Saido Berahino na makosa ya kuunawa mpira katika eneo la hatari.
 
Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO,SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>Zawadi_mawere. Youtube>>>MAWERE TV.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...