15 May, 2015

Petr Cech anaondoka Chelsea? huu ndio msimamo wa klabu yake

cech
Baada ya klabu ya Chelsea kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya England..sasa wameanza mikakati ya kukiboresha kikosi hicho kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu. Kipa wao Petr Cech baada ya kuitumikia klabu hiyo tangu mwaka 2004 uongozi wa timu yake umempa uhuru wa
kufanya mazungumzo na timu nyingine zinazowania saini yake.
Wakala ya kipa huyo Viktor Kolar, amethibitisha kuruhusiwa kufanya mazunguzo kwa mteja wake na timu yoyote inayomuhitaji .
Hivi karibuni Kocha wa Chelsea Jose Mourinho alisema anamuhitaji kipa huyo kuendelea kuitumika klabu hiyo kw amsimu unaokuja na kusisitiza bila uwepo wake klabu hiyo isingeweza kutwaa taji hilo.
Hata hivyo sababu kubwa inayopelekea kipa huyo kuhama ni kucheza Chelsea akiwa chagua la pili huku namba moja akiwa Thibaut Courtois na bosi wake Mourhinho amemtaka hata kama atahama asizichezee klabu za ligi kuu ya England.

Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,SuScribe Youtube>>>MAWERE TV


No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...