15 May, 2015

Unyanyasaji wa watoto umeendelea kuwa sehemu ya matukio ambayo yamekuwa yakikithiri sana ndani ya familia

legs
Unyanyasaji wa watoto umeendelea kuwa sehemu ya matukio ambayo yamekuwa yakikithiri sana ndani ya familia na jamii za watu wengi duniani.Kitendo cha msichana wa kazi kule Uganda kumtesa mtoto wa bosi wake  kwa kumpiga bado hakijasahaulika na mamilioni ya watu duniani baada ya kunaswa na kamera na kusambazwa kwenye mitandano ya kijamii.
Tukio la aina kama hiyo limetokea tena kule Bulgaria baada ya muuguzi Emiliya Kovacheva kumtesa kwa kumpiga mtoto mchanga wa siku nne bila kuwa na huruma kwa madai anapiga kelele.
Mtoto huyo Nicole aliyekuwa ameachwa na mama yake alipata majeraha makubwa kufuatia mateso kutoka kwa muuguzi huyo.
Awali muuguzi huyo alikataa kuwa amefanya kosa hilo lakini baadaye alikiri baada ya kuonyeshwa video baada ya kamera kunasa tukio zima ndani ya humba hicho cha hospitali na kusema alifanya hivyo kutokana na kuchanganyikiwa baada ya mtoto huyo kukataa kulala na kuwasumbua watoto wengine waliokuwa wamelala.
Kwa sasa muuguzi huyo anakabiliwa na kosa la mauaji


Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,SuScribe Youtube>>>MAWERE TV


No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...