01 May, 2015

Mwamuzi mkubwa na mkongwe katika mchezo wa ngumi Kenny Bayless ndiye atakayechezesha pambano la karne

IMG_20150501_101109
Mwamuzi mkubwa na mkongwe katika mchezo wa ngumi Kenny Bayless ndiye atakayechezesha pambano la karne linalosubiriwa kwa hamu kati ya Mmarekani Floyd Mayweather na Mfilipino Manny Pacquiao litakalopigwa katika ukumbi wa MGM Grand Las Vegas tarehe 3 May 2015.

Mmarekani huyo mwenye umri wa miaka 64 ,kwa kuchezesha pambano hilo atapokea kiasi cha dola z kimarekani 25,000 (Paundi 16,600) ambazo ni sawa na Milioni 50 za kitanzania.
Mapambano ambayo Kenny alishawahi kuchezesha hapo awali ni Manny Pacquiao Vs Ricky Hatton,Oscar de la hoyaVs Floyd Mayweather,Ricky Houtton Vs Paulie Malignaggi,Miguel Cotto Vs Antonio Magarito,Manny Pacquiao Vs Miguel Cotto.
Kwa upande majaji ni Burt Clements na Dave Morrett kutoka Las Vegas na jaji watatu ni Glenn Feldmann ,ambao wote ni wazoefu katika kazi hiyo.
Majaji hao wote watatu watapokea kiasi cha dola za kimarekani 20,000 kutokana na kazi yao watayoifanya katika pambano hilo.
Kutokana mapato ya viingilio,televisheni na vyanzo vingine,pambano hilo linataraji kuingiza dola za kimarekani milioni 500 ambapo Floyd Mayweather atapokea dola za kimarekani  Milioni 150 huku Manny Pacquiao atapokea dola za kimarekani  milioni 99 bila ya kujali matokeo.
Mpaka sasa Pacquiao ameshinda mapambano 57 kati ya 64 aliyowahi kupigana huku Mayweather akishuka ulingoni mara 47 na kushinda mara zote

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...