09 May, 2015

Ligi kuu ya Soka Tanzania bara leo imefikia ukingoni

ndanda leo
Ligi kuu ya Soka Tanzania bara leo imefikia ukingoni kwa kushuhudia michezo saba tofauti katika mikoa sita tofauti, huku Mabingwa wapya wa ligi hiyo Dar es salaam Young Africans wakijikuta wanapokea kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Ndanda FC, Mtanange uliopigwa Mtwara katika
Uwanja wa Nangwanda Sijaona.
Kufatia ushindi huo Ndanda wanakuwa wamefikisha pointi 31 na kujiondoa kwenye mkasa wa kushuka daraja.
Uwanja wa Taifa Simba ilikuwa ikiminyana na JKT Ruvu ambapo matokeo yamepatikana kwa Simba kuibuka na Ushindi wa bao 2-1.9
Chamazi jijini Dar es salaam kunako uwanja wa Azam Complex, Wenyeji Azam FC wameweza kutoshana nguvu kwa kugawana pointi na Mgambo JKT baada ya kutoa sare ya bila kufungana.
Shinyanga kwenye Uwanja wa CCM Kambarage kulikuwa na mchezo kati ya Wenyeji Stand United ambao waliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting ambao wameshuka.
Mbeya City ambao walikuwa wakiminyana na Polisi Morogoro kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, Walifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 na kufanikiwa kujikita katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi kuu hiyo ambayo imemalizika leo.mbeta cityKufatia matokeo hayo ya leo Klabu za Polisi Morogoro pamoja na Ruvu Shooting zinakuwa zimeporomoka daraja na kuzipisha timu nyingine nne kushiriki ligi hiyo Msimu ujao.polis mor
Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO,SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>Zawadi_mawere. Youtube>>>MAWERE TV.

TUPATIE MAONI YAKO>>>>







No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...