18 May, 2015

KUTANA NA TETE SI ZILIZOPO KATIKA MAGAZETI YA MICHEZO BARANI ULAYA JUU YA USAJILI BARANI HUMO

GAZETI
THE SUN
Stoke City wamuandilia Begovic mkataba mpya ila kocha wa Stoke City Mark Hughes amesema kwamba maamuzi ya kubaki ndani yani ya timu yako chini ya goli kipa mwenyewe.

DAILY EXPRESS
Kiungo wa Hull city Jack Livermore anaweza kufukuzwa kwenye timu hio baada ya kugundulika kuwa anatumia cocaine kwa mujibu wa vipimo alivyofanyiwa klabuni hapo.
Manchester United wameanza kuonesha nia ya kutaka kuwasajili wachezaji wawil kutoka Roma ambao ni Miralem Pjanic 25, na Radja Nannggolan 27, kwa ada inayokadiriwa kufika £66 million.
Liverpool wanaweza msajili kiungo wa Juventus Andre Pirlo kama ataamua kuihama klabu hio mwisho wa msimu huu. Pirlo mwenye miaka 35 anaweza kuihama klabu hio kwa tetesi kwamba Xabi Alonso anaweza kutua kunako timu ya Juventus.
DAILY MAIL                         
West ham wameamua kuongeza dau lao la kutaka kumwajiri kocha wa Napoli kwa sasa Rafa Benitez, kwa majibu wa klabu ya West Ham Rafa Benitez ndo anashika nafasi ya kwanza katika orodha ya makocha ambao mmoja wapo wanamataka aje kushika nafasi ya Sam Allardcye
Mmiliki wa timu ya Hull city amesema kwamba kocha wa sasa wa timu hiyo Steve Bruce ataendelea kuinoa timu hio hatakama itashuka daraja msimu huu.
THE GURDIAN
Kiungo wa Atletico Madrid Koke amesisitiza kwamba hataihama timu hio msimu huu wala unaokuja japo kua kumekua na tetesi kwamba angeweza kwenda Chelsea wakati wa majira ya joto.
Kiungo wa Everton Kevin Mirallas amesisitiza ya kwamba ana furaha sana ndani ya Everton na hana nia yoyote ya kuihama klabu hio.
THE INDEPENDENT
Kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini amesisitiza ya kwamba mshambuliaji wake hatari raia wa Argentina Sergio Ageuro hato uzwa kwa klabu yoyote ile japo kumekua na taarifa ya kwamba Real Madrid wameonesha nia ya kutaka kumsajili mshambuliaji huyo.
DAILY STAR
Kocha wa Manchester United amemwambia golikipa wake De Gea kua ni mda wa kutoa maamuzi juu ya hatma yake ndani ya klabu kwa msimu ujao.
Dick Advocaat ameaanza maongezi na klabu ya Sunderland kwa ajili ya kuendelea kuinoa timu hio msimu ujao.
Kocha Manuel Pellegrini ana uhakika kua kibarua chake ndani ya Manchester City kipo salama na kua hatukua na haja ya kuonana na wamiliki wa timu hio kwa ajili kuongelea mustakabali wake ndani ya klabu hio.
Arsene wenger amewapa tahadhari wachezaji wake kua kama watakosa kuwemo kwenye tatu bora ya msimu huu basi watakua kwenye wakati mgumu sana kwa msimu utakao anza majira ya joto.
Arsenal, Liverpool na Manchester United wameonesha nia ya kutaka kumsajli mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema, kwa taarifa zilizotoka hivi karibuni uwezekano wa klabu moja wapo kumsajili mshambulijai huyo imeongezeka zaidi baada kuwepo kwa taarifa zingine kuwa Real Madrid wanataka kumuachia Benzema ili wamsajili Alvaro Morata kutoka Juventus.
DAILY TELEGRAPH
Golikipa wa Chelsea Petr Cech anawaniwa na Manchester united kama ikitokea wakamuuza De Gea kwenda Real Madrid.
Kocha wa Manchester United maarufu kama mashetani wekundu Louis Van Gaal amethibitisha kua wameshaanda orodha ya magolikipa ambao mmojawapo anaweza kujaza nafasi ya De Gea kama atajiunga na Real Madrid.


Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,SuScribe Youtube>>>MAWERE TV

 


No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...