21 April, 2015

WEKUNDU wa Msimbazi wamesahau kipigo cha 2-0 walichopata mwishoni mwa juma

Goran-Kopunovic-1024x681
WEKUNDU  wa Msimbazi wamesahau kipigo cha 2-0 walichopata mwishoni mwa juma katika mechi ya ligi kuu Tanzania bara iliyopigwa uwanja wa Sokoine Mbeya dhidi ya wenyeji Mbeya City fc.
Baada ya kucheza mechi 20 Simba ilitangaza kushinda mechi 6 zilizosalia na tayari wameshapunguza mbili ambazo walishinda 2-1 dhidi ya Kagera Sugar uwanja wa CCM Kambarage na nyingine walipoteza Mbeya.
Katika hesabu zao, Simba wamebakiwa na mechi nne tu ili kumaliza msimu huu na mechi hizo ni:
Simba v Mgambo  (Inachezwa kesho Uwanja wa Taifa )
Simba v Ndanda fc  uwanja wa Taifa
Simba v Azam fc    Uwanja wa Taifa
JKT Ruv v Simba  Uwanja wa Taifa
Kocha mkuu wa Simba, Mserbia Goran Kopunovic anaaendelea kukinoa kikosi chake katika uwanja wa Chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM).
Katika mazoezi ya jana, vijana walionekana kuwa na maorali.
Kopunovic alisema: “Tunatumia kipigo cha Mbeya kujiandaa na mechi zijazo. Ligi ina ushindani sana, mechi za Simba ni ngumu, timu zinajipanga sana zinapocheza na Simba, lakini mimi na Matola (Seleman) tunajitahidi kuimarisha kikosi kila siku”.
“Mechi ya Mgambo ni changamoto nyingine, walitufunga kwao (2-0), lakini muda wa kupindua matokeo umefika”.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...