21 April, 2015

Barcelona Vs PSG, Dan Alves anena>>>>

champions-league-badge-preview-barcelona-psg_3293007
Leo usiku vijana wa Enrique watawakaribisha PSG katika mechi ya raundi ya pili ya robo fainali ya kombe la klabu bingwa barani ulaya.
Mechi ya kwanza iliyofanyika pale jijini Paris iliisha huku ikishuhudia wenyeji wakipoteza mchezo ule kwa magoli 3-1
Dan Alves mlinzi wa Barcelona
amewaonya wachezaji wenzaki kupunguza sana lawama hasa kwa waamuzi wanaochezesha mchezo huo.
Hadi sasa timu ya Barca ipo mguu moja ndani na mwingine nje kutokana na ushindi wa mechi yao ya kwanza baada ya kiwango bora cha lius Suarez na kufunga goli 2 ikiwa ni makosa makubwa aliyoyafanya mlinzi wa PSG David Luiz na kuwapa faida timu hiyo ya wakatalunya.
Bao la mwishoni kabisa la kujifunga la mchezaji Jeremy Mathieu ndilo linaloipa matumaini PSG kwa kutakiwa kufunga magoli mawili ili waweze kufuzu.
PSG, ikuwa timu ya kwanza tangu Bayern Munich ilivyofanya hivyo takribani miaka miwili iliyopita kuwapiga Barcelona kwa goli zaidi ya moja nyumbani na kuendelea mzunguko unaofuata na hii itakuwa ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa nusu fainali tangu mwaka 1995.

“hawezi kubashiri matokeokwa sababu hatujui ni nini kitakachotokea ila hatuwezi kubweteka kwa faida ya magoli tuliyoyapata ugenini tutajitahidi kujilinda na kumiliki mchezo kwa kiasi kikubwa kwa kukaa na mpira muda mrefu na kupunguza presha ya wapinzani wetu” alisema Alves kwenye mtandao wa klabu hiyo.luis-suarez-barcelona-psg_3291094
Na kiungo Blaise Matuidi amekubali kwamba yeye na wenzake watakua watajitahidi kufanya mabadiliko na kuwa bora zaidi kuliko walivyofanya katika mechi ya kwanza na kutotoa nafasi ya madhala zaidi kutoka kwa wapinzani wao na watahakikisha wanawatoa mchezoni wakatalunya hao.
“Ni lazima juu ya yote kwenda bila hofu yoyote na kujaribu kila kitu kufikia kile ambacho kitakuwa cha ajabu,” alisema.
“Sisi tuna nia ya kuonyesha kitu cha tofauti na mchezo wa kwanza na hasa kujilina vizuri kwa sababu hicho ndicho kilichokosekana Parc des Princes.” Alisema Matuidi.

Mchezaji wa kimataifa wa Brazil Dan Alves anarudi baada ya kusimamishwa, wakati kiungo Andres Iniesta pia anatarajiwa kurejea baada ya kuumia na kushindwa kuendelea na mchezo Paris.

nahodha wa PSG Thiago Silva atakua nje baada ya kushindwa kupata nafuu kwa muda kutokana na maamuvi ya mguu kutokana na mchezo uliopita,
 
Hata hivyo, kocha Laurent Blanc anapenda kumpa unaodha Zlatan Ibrahimovic na Marco Verratti na wote wanapatikana baada ya wote wawili kukosa mechi ya kwanza kwa baada ya kusimamishwa.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...