11 April, 2015

Klabu ya soka ya Manchester United haitotakiwa kuibeza Manchester City .......

article-3032526-277407F000000578-51_636x455
Klabu ya soka ya Manchester United haitotakiwa kuibeza Manchester City kutokana na matokeo ya siku za mwisho kwao kutokuwa mazuri, na hili alisema Van Gaal.
Kikosi cha mashetani hao wekundu maarufu kwa jina la Red Devils wapo katika maandalizi ya Jumapili kuikabili City kufuatia ushindi mzuri mzuri walioupata siku ya jumamosi dhidi ya Aston Villa wa goli 3-1.
Msimu huu kwa City umekuwa sio mzuri kwao mara baada ya kushindwa kufurukuta katika mechi yao ya mwisho ya ligi kuu kwa kuchapwa na Crystal Palace wakiwa ugenini wa goli 2-1 na kuanza kupoteza matumaini ya kutetea taji la ligi hiyo kama mabingwa watetezi.
Van Gaal amesema aina ya uchezaji wanaocheza City huwa unaleta taabu kwao kutokana na utofauti wa vikosi vyao na hivyo hawana budi kupambana zaidi ili waweze kuendelea kubakia katika nafasi yao ya 3.
” Villa walitumia mfumo wa kujilinda sana lakini sitarajii kwa Manchester City kufanya vile kama Villa walivyotufanyia na pia inahitaji kuwa na ulinzi makini zaidi kwetu” Van Gaal alisema.
” Jumapili tubasubiri tuone kama tunaweza kuendeleza kiwango chetu cha ushindi dhidi ya Manchester Unity” Van Gaal aliongea na Goal.com
Katika raundi ya kwanza ya ligi kuu City walifanikiwa kuifunga United kwa bao 1-0 ambalo lilifungwa na Kun Arguero huku Chris Smalling akienda nje baada ya kupata kadi nyekundu ambapo ilikuwa ni mwezi wa 11.
Van Gaal hakusita pia kuongelea umakini wa wachezaji uwanjani pia akazungumzia ile kadi aliyopata Smalling.
” Mara kwa mara nimekuwa nikilizungumzia hili na katika mechi ya aina kama hizi hatuna budi kuongoza zaidi fikra zetu, tuna kadi 5 nyekundu na hili halijawahi kutokea katika kazi yangu, ni historia” Van Gaal alisema

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...