19 April, 2015

DIAMOND PLUTNUM AWALIPIA WAKAZI 200 WA TANDALE BIMA YA AFYA KWA MWAKA MZIMA

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva ambaye anaendelea kubaki kwenye kilele kila siku, Nasib Abdul aka Diamond Platnumz amejitolea kuwalipia wakazi 200 wa Tandale Bima ya afya itakayo wafanya watibiwe bure kwenye hospitali.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Nasib ameandika haya "...Shukran nyingi ziwafikie Edgepoint Company Ltd kwa kujitolea kunipa Bima ya Afya kwa wakazi 200 wa Tandale, Bima hiyo ambayo itawaruhusu Wakazi hao kutibiwa bure Hospitalini kwa Kipindi cha Mwaka Mzima bure...bima hizo 100 zitaenda kwa Watoto wa shule ya Tandale Magharibi, 50 kwa wakina mama wajane wa Tandale na 50 kwa watoto yatima wa Tandale...Lengo na dhumuni langu si kusaidia Tandale tu, lakini kwakuwa Mwanzo ni mgumu kwa sasa naanzia Tandale ila naamini Wilaya na mikoa Mingine nitafika ku#PushMtaa..."
  

Mawerenewz.blogpot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO,SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA
Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>Zawadi_mawere. AKSANTE.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...