04 March, 2016

Twiga Stars kuivaa Zimbabwe Leo


Timu ya taifa ya Tanzania ya wanawake Twiga Stars leo itashuka dimbani kuchuana na timu ya taifa ya wanawake ya Zimbabwe.
Mchezo huo ni wa kuwania kufuzu kwa fainali za michuano ya kombe la mataifa ya Afrika kwa wanawake.
Mchezo huo utachezwa katika uwanja wa Azam Complex, uliopo Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Waamuzi wa mchezo huo watakua ni Lidya Tafesse, akisaidiwa na Yehuzewdubizua Yehuw, Tsige Sisay, Woinshetkassaye Abera kutoka nchini Ethiopia, huku Kamisaa wa mchezo akiwa ni Geneviev Kanjika kutoka Jamuhuri ya kidemocrasia ya Congo

03 March, 2016

Na huu ni msimamo Ligi kuu Uiengereza

Image result for Epl

English Barclays Premier League

PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Leicester City28169351312057
2Tottenham Hotspur28159449222754
3Arsenal28156744281651
4Manchester City27145848311747
5Manchester United28138737261147
6West Ham United281210642311146
7Stoke City28126103033-342
8Liverpool2711884136541
9Southampton28117103528740
10Chelsea2810994238439
11Everton27911749361338
12Watford28107112929037
13West Bromwich Albion2899102936-736
14Crystal Palace2896133137-633
15Bournemouth2888123244-1232
16Swansea City2879122737-1030
17Sunderland2866163453-1924
18Norwich City2866163153-2224
19Newcastle United2766152750-2324
20Aston Villa2837182251-2916

Arsenal yalala 2-1, Man U na Liverpool zang'ara ligi kuu Uiengereza

TIMU ya Liverpool imeichapa mabao 3-0 Manchester City katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku huu Uwanja wa Anfiled.
Ushindi huo ni sawa na kisasi cha kufungwa kwa penalti 3-1 katika fainali ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup Februari 28, Uwanja wa Wembley baada ya sare ya 1-1.
Katika mchezo wa leo, mabao ya Liverpool yamefungwa na Adam Lallana dakika ya 34, James Milner dakika ya 41 na Roberto Firmino dakika ya 57
Lallana is congratulated by defenders Dejan Lovren and Nathaniel Clyne after putting Liverpool ahead ten minutes before the intervalMan City's England No 1 Joe Hart comes sprawling out of the goal but is unable to deny Milner's shot which hit the post on the way in 


Mchezo mwingine wa Ligi Kuu ya England usiku huu, Manchester United imeendeleza wimbi la ushindi baada ya kuifunga 1-0 Watford, bao pekee la Juan Mata dakika ya 83 Uwanja wa Old Trafford.
Arsenal imefungwa 2-1 nyumbani na Swansea City Uwanja wa Emirates katika mchezo mwigine wa ligi hiyo. Mabao ya Swansea yamefungwa na Wayne Routledge dakika ya 32 na Ashley Williams dakika ya 74, wakati la Gunners limefungwa na Joel Campbell dakika ya 15.

Stoke City imeilaza 1-0 Newcastle United, bao pekee la Xherdan Shaqiri dakika y 80 Uwanja wa Britannia.
West Ham United imeilaza 1-0 Tottenham Hotspur, bao pekee la Michail Antonio dakika ya saba.

Magazeti ya Leo Alhamisi March 3,2016

02 March, 2016

Tambua thamani ya kipaji chako leo.

Image result for TalentMnyonge mnyongeni, haki yake mpeni. Hakika Haja ya mja hunena na Uungwana ni vitendo. Uhali gani kijana mwenzangu? kwanza pole kwa majukumu ya hapa na pale ya kuhakikisha mkono unakwenda kinywani na hata njia ya chooni isiote nyasi. Leo tena kijana wenu nakaa tena jamvini ili niweze kunena la Moyoni hivyo embu na wewe kijana mwenzangu kaa chini tulizungumze hili swala!
Awali ya yote tambua kua Makala hii ni mwendelezo wa makala iliyopita ambayo ilisema Mambo yakufanya wewe kama kijana ili Kufanikiwa katika maisha.
     Nakumbuka wakati nikiwa mtoto niliwahi kuulizwa Mawere ukiwamkubwa unataka kuwa nani? kwangu mimi jibu lilikua nataka kua Mwana sheria. Kwanza kabla yakuendelea, tambua yakua kuna tofauti kubwa kati ya Ndoto na Kipaji, na mara nyinginge mambo haya huenda kwa wakati mmoja ila kwa asilimia chache kwa walio wengi. Wengi tumekua tukiamini kua ndoto ndio kipaji cha mtu ila jambo hili ni uongo mtupu yaani tunajidanganya, ndoto huja baada ya kipaji mfano kama wewe ni mchezaji mpira maarufu, kipaji chako ni kucheza mpira na ndoto yako siku moja ni kuchezea timu ya Taifa, au kama wewe ni mwanamuziki mchanga, kipaji chako ni Muziki na ndoto yako ni Kufanya Muziki kimataifa.
   Mpaka hapo umepata picha ya tofauti kati ya Kipaji na ndoto?
Embu ni kuulize swali , Je unatambua kipaji chako? na kama ni ndio una mpango gani na hicho kipaji cha kipekee ulicho nacho? Utanijibu kupitia anwani yangu ambayo nitakupatia baada ya kunena mawili matatu haya.
post-feature-image     Vijana wengi tumekua tukiishi tuu kama wadudu, unakutana na kijana mtaani kila muda kakalia mambo yasiyo mhusu, mara utamkuta akiongea siasa na huku hata hafahamu chochote kuhusu siasa. Naamini kila mwanadamu kaumbiwa kipaji chake lakini ni wachache wanaweza kutambua vipaji vyao na kuvifanyia kazi kikamilifu na hata leo tumeona matunda ya kazi zao. Mfano mzuri ni wanamichezo wa hapa nyumba kama vile Mbwana samata, Hashim Thabeeti, na wengine wengi wanaong'ara kupitia vipaji vyao. Embu kijana mwenzangu kaa chini na ujitatmini kwa kina na mapana kua wewe ni nan na unataka nini na ufanyeje ili kukikuza kipaji chako.
     Pengine matatizo yako yanayosibu leo ni wewe umeshindwa kutambua kipaji chako na kukiendeleza.. Tatizo hili limetukumba wengi mno, na hii inasababishwa na wazazi wetu, unakuta mzazi anamlazimisha mwanae kufanya kitu ambacho ni nje ya kipaji chake, unakuta mtoto ana kipaji cha kompyuta ama muziki lakini wazazi wanataka mtoto wao awe labda mwalimu au daktari. Kwa kweli hapa ndipo vipaji vya wengi hupotea na kama unavyojua tena mtoto mdogo hukua na kile alichopandikizwa akilini mwake tangu akiwa mdogo, Rai yangu kwa wazazi ni kwamba mtoto ajengwe katika misingi ya kipaji chake, mfano: kama mtoto anapenda muziki na anaonekana kweli ana kipaji cha muziki basi apelekwe katika shule zenye michepuko ya muziki na iwe hiyo kwa vipaji vingine.
       Kwa wale wenzangu na mimi ambao mnafahamu thamani ya vipaji vyenu basi msiishie hapo mlipo embu zidi kuchukua hatua nakusonga mbele na hakika ukijumlisha na bidii utakazo tia utafika ulipotamani kufika wakati ukiwa mdogo.
 NB; Kipaji huendana na ndoto, na bila ndoto hutosonga mbele, msomi mmoja aliwahi kusema " It is not a calamity to die with a dream, but it is a great disaster to die without a dream"  hivyo wenga malengo na ishi katika ndoto zako leo. Acha kupuyanga kila siku katika mabo yasio na msingi.

Kwa leo naomba nikomee hapo na panapo majaliwa week-end hii nitakuja tena hapa jamvini;
Kwa maoni na ushauri usisite kunitumia barua pepe ama ujumbe kupitia:-
 Email: mtokambali2015@gmail.com
 simu namba 0767322193

Rick Ross Is Headed To Trial For Pistol Whipping

Rick Ross press pic via def jamRick Ross will be facing a judge in a case where he allegedly pistol whipped a groundskeeper at his mansion with a Glock.
Ross has countered stating that the man was using is guest house as a venue for cocaine parties. Ross’ lawyers maintain that the rapper was acting in self defense as he encountered intruders on his property. They have yet to contest the actual pistol whipping.
Ross has been indicted on egregious offenses, including kidnapping, aggravated assault, aggravated battery, and possession of a firearm while committing a crime. The original incident started in June 2015.
The trial date has yet to be set.

Download Music: Sauti Sol - Higher-Haiya!

Wimbo umetumbuizwa na Sauti Sol na umeandikwa na wao wenyewe wakishirikiana na Tim Rimbui na kurekodiwa/kutayarishwa na Tim ‘Timwork’ Rimbui wa Ennovatormusic.

Wimbo ni mzuri na ni ukumbusho mwingine kwamba mwanzo mzuri ni kiashirio cha kwanza cha mwisho wake. Ni muhimu kwamba staftahi inatayarishwa kwaajili ya washindi; kwanza tunakuwa hivi tulivyo kwa kile tulichofunguliwa kinywa asubuhi na siku njema huanza asubuhi,” yamesema maelezo ya Sauti Sol.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...