03 March, 2016

Arsenal yalala 2-1, Man U na Liverpool zang'ara ligi kuu Uiengereza

TIMU ya Liverpool imeichapa mabao 3-0 Manchester City katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku huu Uwanja wa Anfiled.
Ushindi huo ni sawa na kisasi cha kufungwa kwa penalti 3-1 katika fainali ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup Februari 28, Uwanja wa Wembley baada ya sare ya 1-1.
Katika mchezo wa leo, mabao ya Liverpool yamefungwa na Adam Lallana dakika ya 34, James Milner dakika ya 41 na Roberto Firmino dakika ya 57
Lallana is congratulated by defenders Dejan Lovren and Nathaniel Clyne after putting Liverpool ahead ten minutes before the intervalMan City's England No 1 Joe Hart comes sprawling out of the goal but is unable to deny Milner's shot which hit the post on the way in 


Mchezo mwingine wa Ligi Kuu ya England usiku huu, Manchester United imeendeleza wimbi la ushindi baada ya kuifunga 1-0 Watford, bao pekee la Juan Mata dakika ya 83 Uwanja wa Old Trafford.
Arsenal imefungwa 2-1 nyumbani na Swansea City Uwanja wa Emirates katika mchezo mwigine wa ligi hiyo. Mabao ya Swansea yamefungwa na Wayne Routledge dakika ya 32 na Ashley Williams dakika ya 74, wakati la Gunners limefungwa na Joel Campbell dakika ya 15.

Stoke City imeilaza 1-0 Newcastle United, bao pekee la Xherdan Shaqiri dakika y 80 Uwanja wa Britannia.
West Ham United imeilaza 1-0 Tottenham Hotspur, bao pekee la Michail Antonio dakika ya saba.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...