21 October, 2016

Mourinho: Pogba apewe muda Man Utd

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amesema hakutarajia Paul Pogba, ambaye alicheza vyema sana dhidi ya Fenerbahce katika ligi ndogo ya Ulaya, azoee soka ya England haraka.
Amesema mchezaji huyo anafaa kupewa muda kuzoea kucheza tena England badala ya kukosolewa kila mara.

Pogba, 23, aliyenunuliwa £89m mwezi Agosti na kuvunja rekodi ya dunia, alifunga mabao mawili Alhamisi wakati wa ushindi wao wa 4-1 dhidi ya Fernabahce.

Hata hivyo hakung'aa Jumatatu dhidi ya Liverpool mechi waliyotoka sare 0-0.
"SIku mbili zilizopita, alitajwa kuwa mchezaji mbaya zaidi katika Lgi ya Premia na saa 48 anasifiwa sana," amesema Mourinho.

"Anahitaji muda. Naridhishwa na uchezaji wake. Ana ustadi tunaohitaji."
Mourinho amesema anaamini Pogba bado anazoa aina tofauti ya soka.
"Niliwa Italia na nafahamu sifa za soka huko, kasi yake na ukali wake," Mourinho, 53, alisema.

"Kuwa Italia kwa miaka minne au mitano na kisha urejee Ligi ya Premia, sikumtarajia aanze mara moja kung'aa."

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...