04 October, 2016

Fifa kuongeza timu zitakazoshiriki kombe la dunia Kufikia 48

Gianni Infantino
Rais wa Fifa Gianni Infantino ameshauri kuongezwa wa timu zinazoshiriki kombe la dunia na kufikia 48 zaidi ya ahadi yake aliyoitoa wakati akiwania nafasi hiyo kuwa atafikisha timu 40.

Anashauri kuwa timu 16 kati ya zote zitatolewa katika hatua ya awali kabisa.
Kisha kubaki 32 zitakazoendelea katika makundi baada ya hatua ya mtoano kukamilika.

Infantino anasema kuwa mapendekezo hayo yatapelekwa katika bodi ya Fifa Januari.
''Haya ni mawazo ya kupata suluhisho la uhahika, tutayajadili mwezi huu na kufahamu nini cha kufanya mwaka 2017,'' alisema Infantino mwenye miaka 46.
Infantino aliingia madarakani kuliongoza shirikisho hilo la Fifa mwezi Februari baada ya kujiuzulu kwa Sepp Blatter.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...