20 September, 2016

Snura: Mimi ni Malkia Wa uswazi

Mwanamuziki na Muigiazajia Snura amejipa cheo cha malkia wa Uswazi kwa madai  kwamba amekulia maisha ya Uswahilini, hata nyimbo anazo imba zina maudhui na mazingira ya Uswahilini, hivyo ni sahihi kujiita jina hilo.

"Mimi ni Malkia wa Uswazi, kwanza nmekulia huko, nimekaa huko, na hadi sasa nakaa huko na nyimbo zangu ni za uswazi, hivyo sioni kama kuna shida nikijiita Malkia wa Uswazi" -Alisema Snura.

Snura alisema hayo kwenye kipindi cha eNewz na kufafanua kuwa hajali kwamba ataelewekaje,  kwa madai kwamba hata mashabiki  wanamuita kwa jina hilo na Pia ndiye Malikia wa Kisingeli kutokana na Muziki anao fanya.
Nyota huyo alisema hata kama yupo mwanamuziki mwenzake Shaa, ambae kwanzia hapo awali alikua akijiita jina hilo na kudai kwamba watu tuu wenyewe wanajua tu nani Malkia wa Uswazi.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...