22 August, 2016

Semenya,Mo Farah na Brazil wawika Rio

Caster Semenya ashinda dhahabu

Mwanariadha wa Afrika Kusini Caster Semenya amejishindia dhahabu katika mbio za mita 800 .
Franchine Niyonsaba amechukua nafasi ya pili na kujishindia medali ya fedha huku mkenya Margeret Nyairera Wambui akichukua medali ya shaba .

Semenya alivunja rekodi ya taifa lake katika mbio hizo na kuweza kushinda kwa dakika moja dakika 55 na sekunde 28.
Mohammed farah

Mwanariadha huyo ambaye alizua utata mwaka 2012 alipofanyiwa ukaguzi wa kijinsia alijishindia fedha mwaka huo.
''Ndoto ya mwanariadha yoyote ni kushinda dhahabu hususan katika mbio za Olimpiki'',alisema Semenya.
Na Marekani imeshinda mbio za mita 400 mara 4 kupokezana vijiti kwa wanawake na kujinyakulia nishani ya dhahabu, baada ya kutimka kwa muda wa Sekunde 19.06.

Kina dada hao wameandikisha ushindi mara sita mtawalia katika mashindano ya Olimpiki.
Kikosi cha kina dada kutoka Jamaica kilizoa fedha, ilhali Uingereza ikajipatia nishani ya shaba.
Kikosi cha wanaume pia cha Marekani kimeshinda mbio za mita mia nne mara nne kupokezana vijiti.
Naye mwanariadha wa Uingereza Mohammed Farrah, ameandikisha ushindi mara mbili katika mbio ndefu za mita elfu kumi na elfu tano mtawalia, huku akizoa dhahabu baada ya kuwapiku wenzake kwa kasi huko Rio de Janeiro. 

Miaka minne iliyopita alizoa dhahabu mbili katika mbio hizo hizo, katika mashindano ya Olimpiki Jijini London.

Wakati huo huo, timu ya soka ya wenyeji Brazil, inafurahia nishani yake ya kwanza ya dhahabu, katika soka.
Mabingwa hao mara tano wa kombe la dunia waliwanyuka Wajerumani katika mikwaju ya penalti, baada ya mechi hiyo kumalizikia bao moja kwa moja, hata baada ya kipindi cha ziada

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...