13 May, 2016

Sema naye, mwambie ukweli usimwogope.

Habari gani mpendwa msomaji wa Mtokambali? week-end ndiyo hiyoo imekwisha fika na kama ilivyo ada lazima tabasabu litawale kwa baadhi ya wafanyakazi ambao hawakupata muda wa kupumzika kwa takribani siku tano.

Leo nmepanda hapa MTOKAMBALI nikiwa na swala moja tuu ambalo mara nyingi hunitawala katika fikra zangu na hata kuyaona kwa macho yangu na jambo hilo ni "Uoga katika kumwambia mtu Ukweli ama la Moyoni"

Kuna wale vijana wenzangu mtaani huwa naonaga wakiitwa Madomo zege na Wengine niliwahi kusikia wakiitwa nyoka Kibisa(Yaani hawana sumu), nashindwa kutambua hali hii maana nakuawa na maswali mengi kichwani juu ya jambo hili yakwamba Je ni uoga wa kumwambia mtu? je ni Aibu ya kumwambia mtu kitu? ama je ni nini hasa kinachomfanya mtu kuwa katika hali hiyo?(Embu tuongee kidogo hapa)

 Leo acha nikuambie ndugu yangu...

Nafahumu kwamba moyo wa mtu siyo wa chuma bali ni nyama, na kila mwanadamu ana haki ya kupendwa na hata kupenda pia.. ila linapo kuja swala la Mapenzi moyo huo huo hujeuka sega la asali ama kujeuka chungu kama shubiri na ndivyo mapenzi yalivyo.

Ila kwa kuwa tumeumbiwa kupenda, hatupaswi kuunyima moyo kile unacho stahili, sasa je ni kwa nini uogope kuuupatia moyo kile unacho kipenda? Je hufahamu kwamba faraja na furaha huja kutoka moyoni?

Kuna wale vijana wenzangu ambao humpenda mtu kwa dhati kabisa na hata kudhamiria kuwa na mtu fulani katika maisha yake ila anaogopa kumwambia mtu yule. Na hii nimeiona hasa kwa Vijana wa kiume, mara nyingi wamekuwa wakitamani kuwa na wachumba wazuri wenye hadhi flani ila wamekuwa wakijikuta katika wakati mgumu pale wanapo taka kufunguka.

 Utakuta mtu ana maswali meengi katika moyo wake kwamba je atanionaje? je si atanitukana? je si atanikataaa?

Kakuambia nani kwamba yule unaye mtaka takufanyia hayo unayowaza? Ndiyo yawezekana ukaambiwa hayo maana kuna watu wengine huwa na hulka ya kujiskia kwamba wao ni bora zaidi ila kabla hujafikia huko na wewe jiulize je ukimwambia na akakubali utajiskiaje?(Aibu ama furaha?)

Na ndiyo maana leo hii nakupa mambo kadhaa ya kufanya ili kuondokana na hiyo hali na mwishoni kupata kile ulicho kitamani katika maisha yako.

1.Acha kuwa na maswali mengi yasiyokuwa na majibu 

Yale maswali ya Atanionaje, hatanitukan? hatani fanyeje tafadhali yawekwe pembeni. Acha nikuambie tuu ukweli mpenzi msomaji, hakuna jambo linalo umiza katika ulimwengu wa leo kama Mapenzi. Mapenzi upofu, mapenzi ukichaa mapenzi uchizi. Ukitaka kumla bata uache kumchunguza.

2.Funguka mbele ya macho yake (say it to his/her face)

Kipekee mimi huwa napenda mtu ambaye huniambia hisia zake mbele ya uso wangu kuliko yule anaye tumia njia kama simu ama njia nyingine ile. Watu wengi pia hupenda hivyo, na kwa maana hiyo basi huna budi kutenga muda wako na kukutana na mtu ambye unampenda ila unaogopa na kisha mwambie.

3.Jiamini.

Kitika mapenzi bwana hakuna mambo ya uoga, wewe kuwa jasiri na kujiamini kisha mfute na kumwambia ukweli juu ya moyo wako, mweleze na yeye atakusikiliza bila hiyana.

4.Kuwa muwazi.

Unajua ni bora kuwa muwazi wakati wote maana watu watujua namna ya kukusaidia kuliko kuficha ficha mambo na mwisho wa siku unaumia moyo wako bure pasipo kuwa na msaada.

5.Usi sikilize ya watu we fanya yako.

Japo unapaswa wakati mwingine kusikiliza watu wana sema nini, ila wakati mwingine hupaswi kuyasikiliza maana ya mwanadamu ni mengi na mengine ni yakuvunja moyo. Nafahamu kuna vijana wengine kazi yao ni kuvunja vijana wengine moyo hachelewi kukuambia yule mwanamke ni Malaya, mhuni ama nini. Kwa namna hiyo basi jiepushe na hali hiyo.


Kwa kusema hayo nimalizie kwa kusema "Usione sooo sema nae, mwambie ukweli. Tukutane tena hapa hapa Mtokambali nyumba ya maajabu na visa, mtaa wa burudani na hamasa kwa vijana.

 


Jiunge na watu 3000 walio chagua kujiunga na MTOKAMBALI ili uweze kujipatia Makala zetu kila ifikapo week-End moja kwa moja kwenye simu yako BURE!

* inahitajika


No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...