22 February, 2016

Nywele yauzwa kwa dola 35,000!

Shungi la nywele ya msanii nguli wa muziki chapa Rock na muanzilishi wa kundi la ''The Beatles'' John Lennon aliyeaga dunia miaka 36 iliyopita imeuzwa kwa dola elfu thelathini na tano ($ 35,000) katika mnada mmoja huko Marekani.
Kinyozi wa Muimbaji huyo maarufu kote duniani alificha shungi la nywele baada ya kumnyoa msanii huyo alipokuwa akijiandaa kuigiza katika filamu moja.
Lennon aliuuawa mwaka wa 1980 mjini New York Marekani.
Mnunuzi mmoja shabiki sugu wa Lennon kutoka Uingereza ndiye aliyeandika hundi hiyo ya dola ($ 35,000).
Bidhaa zingine zilizotumika na kundi hilo la muziki la ''The Beatles''pia ziliuzwa katika mnada huo huko Texas.
Baadhi ya bidhaa hiyo ilikuwa nakala maalum ya albamu yao ya 'Yesterday and Today', iliyouzwa kwa dola laki moja u nusu ($150,000).

CHANZO; BBC

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...