17 February, 2016

Marekani na Cuba zimetiliana tena saini makubaliano ya kurejesha tena safari za ndege za abiria baina ya nchi hizo mbili


Marekani na Cuba zimetiliana tena saini makubaliano ya kurejesha tena safari za ndege za abiria baina ya nchi hizo mbili kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka hamsini iliyopita.
Utiwaji wa saini ya makubaliano hayo ulikuwa ni baina ya waziri wa usafiri wa Marekani , Anthony Foxx na mwenziwe kutoka Cuba Adel Izquierdo Rodriguez, mjini Havana makubaliano hayo yatashuhudia safari lufufu za kila uchao baina ya mataifa hayo yaliyokuwa mahasimu hapo awali.
Matarajio ya kuanza kwa safari hizo ni baada ya mwezi mmoja,ingawa mpaka sasa kisheria ni Marufuku kwa raia wa Marekani kuitembelea Cuba kama mtalii.
Ki diplomasia uhusiano wa nchi mbili hizo ilianza kurejea zaidi ya takribani mwaka mmoja uliopita .Mwandishi wa BBC aliyeko mjini Havana ameelezea juu ya makubaliano hayo ya hivi karibuni kwamba yamekuja baada ya ikulu ya Marekani kutafakari uwezekano wa safari za kiserikari za rais wa Cuba nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...