22 January, 2016

JINSI YA KUISHI NA MWANAUME/MKE MWENYE GUBU.

how to deal with nagging spouse 8020fashions 3
John ana mke ambaye haoni uzuri wa kitu chochote anachofanya, akifika tu nyumbani mke wake huanza kumlalamika kuwa hela anayoacha nyumbani haitoshi, au akichelewa kurudi mke wake humsingizia John kuwa ana wanawake wengine huko nje ndio kisa cha kuchelewa kurudi nyumbani, hata John akitoka na marafiki pia ni tatizo kubwa.
John anasema muda mwingine anatamani hata aanze kumpiga mke wake kwakuwa mambo anayolalamika au anayoyasema si ya kweli. Mke wake anashindwa kuuliza maswali kwanza bali anaanza kulalamika na kumsingizia vitu vingi.
John anasema alianza pole pole kufanya vitu mke wake alivyokua akimsingizia kwani alianza kuchelewa kurudi nyumbani ili asikutane na mke wake, na baadaye akapata mwanamke mwingine na kuanza kunywa pombe.
John anasema matendo aliyoyafanya yalifanya ndoa yake izidi kuharibika na mke wake ndio alizidisha gubu.
Hili jambo hutokea sana kati ya wanandoa na sio mwanamke tu anayekua hivo, hata wanaume nao, Gubu, malamiko lazima itatokea katika mahusiano, inategemea tu ni jinsi gani mnaweza kuihandle na kuzuia matatizo makubwa zaidi.
how to deal with nagging spouse 8020fashions
JINSI YA KUISHI NA MWANAUME AU MKE MWENYE GUBU sio rahisi lakina inawezekana,
  • Kwanza kabisa unatakiwa uwe msikivu, hili tatizo linaanza pale mwanaume/mke akiwa na malalamiko lakini mwenzako hawi msikivu. Hii itapelekea mwenzako kuona kuwa huna time naye na hujali vitu anavyokwambia, na hivyo huyo mtu ataanza kulalamika na kufiria sababu zingine kabisa za kwanini humsikilizi kama vile kuwa na mpenzi mwingine nje ya mahusiano yenu.
how to deal with nagging spouse 8020fashions 4
  • Jaribu kuwa muelewa, kama mambo yameshakuwa mabaya kati yenu jaribu kuwa muelewa, acha kujibu malalamiko ya mwenzako kwa kufoka au kwa vurugu. Jaribu kufikiria ni kitu gani kinachomfanya mwenzako awe hivo na kuongea nae.
  • Kwa wanawake mpunguze dharau, hasira na malalamiko yasiyo na mbele wala nyuma kwa waume zenu, na msizue matatizo yalipita. Focus katika tatizo lililopo ili muweze kulisolve.
  • Kwa wanaume, mnatakiwa kuwasikiliza wake zenu, sikiliza malalamiko waliyokuwa nayo, myaongelee na kuyasolve matatizo.

Young couple has breakfast at italian café
Wanandoa wakishindwa kutatua matatizo kama haya, chuki inakua kati yao na ndoa inazidi kuwa chungu, na matumaini ya kusolve matatizo kati yao yanakuwa hamna tena, na hii inaweza kuwa mwisho wa mahusiano yao.
Wewe je, unaishi na mwanaume au mwanamke mwenye gubu? Unawezaje kuishi nae, au unafanya nini ili kuweza kumhandle na kuepuka matatizo kati yenu?

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...