19 December, 2015

Miaka 9 ya Wayne Rooney na Man United

Nahodha wa Manchester United Wayne Rooney leo anatarajia kutimiza mechi yake ya 500 tangu alipoanza kuitumikia klabu hiyo mnamo 2004.
 
Rooney anatarajiwa kurejea dimbani leo baada ya majeruhi ya enka yaliyomuweka nje katika mechi 3 dhidi ya  West Ham, Wolfsburg na Bournemouth.
Rooney alijiunga na  United kutoka Everton mwaka 2004 kwa ada ya uhamisho ya £25.6m akiwa na miaka 18 na katika mechi yake ya kwanza tu alifunga hat trick yake ya kwanza katika ushindi wa 6-2 vs Fenerbahce.
 
Mshambuliaji huyo mpaka sasa ameshashinda makombe matano ya EPL na moja la Champions League, na tuzo kadhaa zake binafsi.

Wayne Rooney ameshacheza mechi 499 akiwa na jezi za mashetani wekundu, akishika nafasi ya 10 katika listi ya wachezaji waliocheza mechi nyingi zaidi katika historia ya klabu hiyo.


Mpaka kufikia sasa Rooney ameshafunga jumla ya magoli 237 katika mechi 499, katika magoli hayo – amefunga hat trick mara 8.
 Klabu ya Aston Villa ndio timu ambayo Rooney ameifunga magoli mengi zaidi tangu alipoanza kuitumikia United. 
Wayne Rooney amefunga magoli 11 katika mechi 24 vs Manchester City. Idadi hii inamfanya kuwa mchezaji aliyefunga magoli mengi zaidi kwenye Manchester Derby – Baba Kai pia ana rekodi ya kutoa assists 82 katika premier league tu.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...