25 December, 2015

post-feature-imageJeshi la Polisi mkoani Arusha linawashikilia watu wanne wakiwemo mke wa marehemu dereva na mtunza bustani kwa tuhuma za mauaji ya aliekuwa mkuu wa kitengo cha ulinzi na usalama wa shirika la hifadhi za Tanapa Emili Kisamo aliyeuwawa kwa kukatwa shingo na kutelekezwa ndani ya gari lake Nissan Mazda No T 435 CSY eneo la Lemala jijini Arusha tarehe kumi na nane ya mwezi huu.

Kamanda Polisi mkoa wa Arusha Lebaratus Sabas amesema baada ya tukio hilo jeshi la polisi lilifanya uchunguzi na kuwakamata watu hao lakini mtunza bustani Ismail Swalehe amekiri kufanya mauajki hayo kwa tamaa ya fedha kiasi cha shilingi milioni tano na kati ya hizo milioni nne zimepatikana zikiwa zimefukiwa chini nje ya nyumba ya marehemu na kudai alimkata shingo kwa panga akiwa sebuleni  anakunywa uji ili aweze kuelekea kazini.

Kamanda Sabas amesema uchunguzi wa jeshi la polisi pia umegundua panga moja liliokuwa na damu ambalo lilikutwa kwenye stoo ya nyumba ya marehemu vitu vingine ni taulo nne kitambaa cha mezani suruali ya mtuhumiwa ambazo zilifichwa kwenye migomba karibu na banda la kuku nyumbani kwa marehemu ambazo zinadaiwa ndiyo zilizo tumika kupigia deki baada ya kuuwawa.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...