24 August, 2015

Waliotibua shambulizi watuzwa Ufaransa


Rais wa Ufaransa Francois Hollande amatoa tuzo la juu zaidi nchini Ufaransa kwa Waamerika wanne ambao walitibua shambulizi la kigaidi kwenye treni ya mwendo wa kasi kwenda mjini Paris siku ya Jumamosi.
Mwanajeshi Mmarekani ambaye alijeruhiwa Spencer Stone alipomuangusha mwanamgambo huyo sakafuni , alipewa tuzo hilo pamoja na Waamerika wengine na Muingereza mmoja ambao wote wametajwa kuwa mashuja.
Bwana Hollande alisema kuwa kungetokea maafa kwenye treni hiyo iwapo abiria hao hawangechukua hatua.
Waziri mkuu wa Ubelgiji Charles Michel na balozi wa Marekani nchini Ufaransa Jane Hartley walishudhuia sherehe hizo.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...