28 August, 2015

Ulikua unafahamu kama Chris brown anamiliki migahawa 14 ? Soma hii



Pamoja na kupata mafanikio makubwa kwenye music akiwa kama mmoja ya wasanii wanaouza zaidi, Christopher Maurice Brown au maarufu kama Chris Brown pia ni mjasiliamali na anamiliki migahawa 14 inayouza Burger na vyakula vya haraka (burger kings).
Chris brown ameshare mambo 25 ambayo watu hawafahamu kuhusu yeye  “25 Things You Don’t Know About Me” ya mtandao wa US Weekly na moja ya mambo hayo ni kuwa anamiliki migahawa 14 au maarufu kama Burger Kings.
Kumiliki migahawa inayouza vyakula vya haraka ni moja ya biashara yenye mafanikio makubwa Marekani lakini sio rahisi, kwa mujibu wa Burger kings mtu yoyote mwenye nia ya kufanya biashara hiyo anatakiwa awe na mtaji wa dolla  1,500,000 na nyinine dolla 500,000 kwa ajili ya vinywaji (Hii ni kwa mgahawa mmoja)  Chris brown anamiliki migahawa 14, unaweza piga hesabu.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...